Sunday, October 1, 2023

KAMATI NA KAZI ZAKE

Uongozi wa Kundi

Wafuatao ni Viongozi Waanzilishi wa Kundi ambao wamekuwepo toka kuanzishwa kwa Kundi mwaka 2010 hadi sasa;

  1. Martin Kessy kutoka Jimbo Kuu Katoliki la Arusha…. Mwenyekiti
  2. Ignace Massao kutoka Jimbo Kuu Katoliki la Dodoma ….Makamu Mwenyekiti
  3. Anna Jensen Msowoya kutoka Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam…..Katibu Mkuu
  1. Josephine Kajembe kutoka Jimbo la Dar es Salaam -Katibu Msadizi
  2. Salome Ng’ingo kutoka jimbo la Dar es Salaam – Katibu Msadizi
  3. Catherine Patrick kutoka Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam…..Mweka Hazina
  4. Prosper Magali kutoka Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam….. Msemaji wa Kundi na Kiongozi wa Shughuli za Kijamii
  5. Majegero Selecius na Nicolaus Mtakingilwa kutoka Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam…… Wasimamizi na Waongozaji Kundi Mtandaoni (Group Admins/Directors)

 Walezi wa Kundi

Baba Benno Kikudo kutoka Parokia ya Kibaha, Jimbo Kuu la Dar es Salaam amechaguliwa Mlezi Mkuu akisaidiana na Baba Timothy Maganga wa Parokia ya Bikira Maria Mama wa Huruma, Mbezi Beach, Jimbo Kuu la Dar es Salaam.

Sababu za Mababa hawa kupendekezwa kuwa Walezi ni pamoja na

  1. Wanapatikana mara kwa mara kwenye mitandao
  2. Wanafahamu mengi kuhusu mitandao ya kijamii
  • Wapo karibu sana na vijana na wanaelewa vizuri mahitaji ya vijana
  1. Wapo tayari muda wowote kukutana na kushauriana na vijana

Mapendekezo ya Marekebisho ya Muundo na Kanuni za Uendeshaji wa Kundi

  1. Mapendekezo ya Kuwepo kwa Kamati Mbalimbali

Zifuatazo ni Kamati ndogo zinazopendekezwa kufanya kazi na Viongozi wakuu wa kundi ili kuleta ufanisi katika utendaji kazi;

i)   Kamati Tendaji

Kamati Tendaji itaundwa na Mwenyekiti, Makamu Mwenyekiti, Katibu na Katibu Msaidizi, Mweka Hazina, Msemaji Mkuu, Wenyeviti wa Kamati Mbalimbali na Wanachama Waanzilishi wa Kundi.

Majukumu ya Kamati Tendaji ni

  • Kusimamia mambo yote ya kundi pamoja na ushauri kwa kamati zote
  • Kupokea taarifa mbalimbali za kamati na kuzitolea
  • Kuandaa kalenda ya taratibu mbalimbali za chama
  • Kuwa mwakilishi wa kundi sehemu yeyote kundi linapohitajika
  • Kupokea na kutoa ushauri panapotokea kukinzana kwa wanachama au kamati ndogo ndogo
  • Kuwa ni wasemaji wakuu wa
  • Kuteua viongozi waandamizi wa kundi (Katibu, Katibu Msaidizi, Mwekahazina, Msemaji Mkuu wa Kundi, Viongozi na wajumbe wa Kamati Mbalimbali) kwa kuzingatia sifa zinazohitajika kwa ngazi husika
ii)   Kamati ya Kuratibu Shughuli za Mitandao

Kazi ya kamati hii ni kuratibu shughuli zote zinazofanywa na kundi ikiwa ni pamoja na;

  1. Kuwa waendesha na wasimamizi wa shughuli za mitandao (Admins)
  2. Kuratibu zoezi la kuunganisha wanachama wapya kwenye mitandao
  3. Kuposti matukio na shughuli zote za utume kwenye mitandao
  4. Kufuatilia kila wakati kadiri iwezekanavyo matukio yanayoendelea kwenye majukwaa yote ya kundi mitandaoni na kuchukua hatua stahiki mara moja kunapotokea jambo linalokwenda kinyume na maadili ya kundi

Wafuatao wanapendekezwa kuunda kamati hii

  1. Majegero Selcious……….. Mwenyekiti
  2. Pauline Mlekani…………. Katibu
  • Julian Mosha…………….. Mjumbe
  1. David Kiwasila………….. Mjumbe
  2. Nicholaus Mtakingilwa …Mjumbe
  3. Gordhard………………….. Mjumbe
  • George Nkana……………. Mjumbe
  • Albert Byengello………. Mjumbe

Kamati hii itasimamiwa na Makamu Mwenyekiti

iii) Kamati ya Kuratibu Matendo ya Huruma

Kamati hii itawajibika kuratibu zoezi zima la kusaidia wahitaji mara mbili kila mwaka kipindi cha kwaresma na kipindi cha majilio. Kazi ya kamati hii pamoja na mambo mengine ni;

  1. Kutafuta maeneo yenye mahitaji popote pale Tanzania na kufahamu mahitaji katika eneo husika
  2. Kusimamia uchangiaji kwa ajili ya kufanikisha matendo ya huruma
  3. Kuhamasisha michango kutoka kwa wanachama na wasio wanachama
  4. Kuratibu safari za matendo ya huruma

Kamati itafanya kazi kwa karibu na Uongozi Mkuu au kamati ndogo itakayoteuliwa au Mwanachama Mwakilishi kwenye Jimbo au Parokia ambayo tukio litaenda kufanyika.

Wafuatao wanapendekezwa kuunda kamati hii

  1. Alfred Lupogo…………. Mwenyekiti
  2. Angella Assenga………. Katibu
  • Veritasi Nderumaki….. Mjumbe
  1. Salome Ng’ingo……… Mjumbe
  2. Hellena Chitukuro……. Mjumbe
  3. Salvina Kyaduma…….. Mjumbe

Kamati hii itasimamiwa na Mweka hazina.

iv) Kamati ya Kuratibu Shughuli za Pamoja na Utume wa Utoto Mtakatifu

Baada ya shughuli za pamoja kati ya Kundi letu na Utume wa Utoto Mtakatifu Jimbo Kuu la DSM kufanyika kwa mafanikio haswa baada ya shughuli za kundi kutambuliwa na Mwashamu Polycarp Kardinali Pengo, Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu la DSM, inapendekezwa sasa mtazamo huu uenee mahali pote ambapo kundi lina wanachama. Lengo la ushirikiano huu ni kuhakikisha kwamba kundi linashiriki malezi wa watoto ndani ya kanisa ambao ndio baadae watakuwa wanachama wapya wa kundi na wajenzi wa kanisa la baadae.

Kwa hiyo inapendekezwa kuwepo kwa kamati itakayokuwa ikifanya kazi kwa karibu na Utume wa Utoto Mtakatifu kwenye Majimbo na Parokia waliko wanachama.

Kazi ya kamati hii ni pamoja na;

  1. Kushiriki vikao vya pamoja vitakavyoitishwa kwa ajili ya kuratibu shughuli mbalimbali za utume
  2. Kushiriki mialiko mbalimbali ya utume itakayoletwa kutoka Utoto Mtakatifu
  3. Kufanya na kushiriki mambo mengine ya ushirikiano na Utoto Mtakatifu kama yatakavyokuwa

Kwa kuanzia, Kamati ya Jimbo la DSM itaundwa na utaratibu huu utaendelea katika Majimbo mengine kadiri ya mahitaji.

Wafuatao wanapendekezwa kuunda kamati ya Jimbo la DSM

  1. Winnie Moshi….. Mwenyekiti
  2. Antonia Ilomo….Katibu
  • Veronika Msabaha…..Mjumbe
  1. Jane Msilu….Mjumbe
  2. Einhard Mbuge…. Mjumbe

Kamati hii itasimamiwa na Msemaji Mkuu

v) Kamati ya Kuratibu Shughuli zote za Kiroho (Liturjia)

Pamoja na mambo mengine, shughuli za kiroho zitakuwa msingi wa maendeleo ya kundi. Hivyo basi kamati hii itakuwa na jukumu la;

  1. Kuandaa matamasha, makongamano, semina, mafungo, maungamo, misa n.k kwa ajili ya wanachama ili kujenga afya ya kiroho ya wanachama
  2. Kuratibu mafunzo ya kiroho kwenye mitandao kwa kushirikiana na kamati ya

Kamati hii itaundwa na wafuatao

i Br Lionel Sitta………… Mwenyekiti

  1. Bertha Fred……………. Katibu
  • Josephine Kajembe…Mjumbe
  1. Catherine lacha……… Mjumbe
  2. Prosper Magali………. , Mjumbe
  3. Helena Turuka……….. Mjumbe
  • Anitha Mwoleka……Mjumbe

Kamati hii inasimamiwa na Baba Mlezi wa Kundi