LEO Alhamisi, Machi 17, 2022 ni siku ya kumbukizi ya kifo cha aliyekuwa Rais wa Awamu ya 5 wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Hayati Dkt. John Pombe Magufuli. Kumbukizi hiyo inafanyika kitaifa katika Viwanja vya Magufuli, Chato mkoani Geita ambapo Rais Samia Suluhu Hassan anawaongoza Watanzania kumkumbuka na kumuenzi kiongozi huyo shujaa.