Mhasham Baba Askofu Mkuu Beatus Kinyaia OFM Cap.  Leo ameongoza Ibada ya Misa Takatifu ya Ufunguzi wa maadhimisho ya miaka 10 ya utume wa Wamisionari Wakatoliki Mtandaoni, Aidha Askofu Kinyaiya amepongeza juhudi za kweli zinazofanywa na mchepuo huu wa vyama vyama vya kitume , Katika  mahubiri yake  baba Askofu Kinyaia  alitoa   mfano wa MAJI.

Maji yana viumbe wengi waishio.

Kuna viumbe hai na ambavyo sio Hai lakini pia kuna takataka nyingi pia ambazo zipo kwenye maji. (maji akimaanisha Dunia au Ulimwengu ambapo sisi tupo ndani yake.)

Lakini katika maji kuna viumbe wazuri na wabaya , Maji na viumbe wake ni kama mwanadamu na mitandao ya kijamii, mitandandao ya kijamii inaweza fanyakazi kwa kuelimisha au kupotosha jamii.

Kundi la  Wamisinari Wakatoliki Mtandaoni  waliona fulsa  hii ya mitandao na kuamua kulipeleka huko neon la Mungu.

Takataka ni yale mengi yanayopostiwa kwenye hiyo mitandao ambayo hayana maadili katika uhai wa kiroho.

Aidha Misa hiyo Takatifu  iliyoongozwa  na  Mhasham Baba Askofu pia ilikuwa inarushwa live (Mubashara ) na Group ya Facebook   wamisionari wakatoliki mtandaoni  Pamoja na Redio Maria

Hata hiyo wamisionari waalishukuru kwa baba Aaskofu Kinyaia kwa utayari wake kuwa Askofu  mweyeji wa maadhimishi hayo na pia kuwa tayari kuendesha  Ibada ya misa Takatifu  ya Ufunguzi.

Baada ya misa wamisionari walimkabidhi baba askofu kiasi cha Tsh 4,500,000/= kama Matendo yao ya Huruma kwa ajili ya kumsaidia baba Askofu kusomesha waseminari wanaohudumiwa  na J imbo

Wamisionari wakatoliki mtandaoni pia walitumia fulsa hii kumuomba baba Askofu kuzindua kitabu cha historia ya miaka 10  ya wamisionari wakatoliki mtandaoni Tanzania  katika uinjilishaji

Baada ya misa Baba mlezi wa wamisionari kitaifa baba Padre Thimoth Nyasulu Maganga alitoa neneo la shukrani

Baadae makamu mwenyekiti Taifa kwa Niaba ya Mwekiti taifa Alitoa neneo la shukrani

Pia msemaji wa wamisionari alipata muda wa kusema neneo

Misa hiyo iliongozwa kwaya ya Mwenyeheri Maria Ledochowska  wa parokia ya kiwanja cha Ndege Dodoma.