Wamisionari Wakatoliki Mtandaoni na wageni waalikwa leo Novemb 11, 2020 kuanza kuwasili jijini Dodoma tayari kwa ajili ya maadhimisho ya miaka kumi  10 ya utume wao.

Majimbo mbalimbali Katoliki Tanzania watashiriki Maadhimisho hayo yatakayo funguliwa rasmi kwa Misa ya Ufunguzi na Mhashamu Baba ASKOFU  BEATUS   KINYAIA  WA JIMBO KUU KATOLIKI LA DODOMA  KATIKA KANISA KUU LA KIASKOFU  LA MTAKATIFU   PAULO   WA  MSALABA  12.11.2020. (MISA ITAANZA SAA TATU ASUBUHI)

Baada ya Misa ya Ufunguzi, Kutafuatiwa  na   Semina   zitakazofanyika  katika ukumbi wa Kanisa la Kirutheli Karibu Kabisa na Kanisa Kuu Katoliki la Dodoma (Cathedral)

Pia katika maadhisho hayo mitandao ya kijamii ya Wamisionari Wakatoliki Mtandaoni inayofanya shughuli za uinjilishaji itazinduliwa rasmi.

 

Wamisionari Wakatoliki Mtandaoni wanatumia mitandao ifuatayo katika kusafirisha ujumbe wa Neno la Mungu.

 

1.Facebook Group – WAMISIONARI WAKATOLIKI MTANDAONI

2.Facebook Page – Wamisionari Wakatoliki Mtandaoni

3.Istagram – Wamisionari Wakatoliki Mtandaoni

4.Twitter –  Wamisionari Wakatoliki Mtandaoni

5.Telegram – WAMISIONARI  WAKATOLIKI  MTANDAONI

  1. Website:    www.wamisionariwakatoliki.or.tz

Pamoja na tukio hilo pia  kutakua na tukio la kuzindua Kitabu cha Historia cha Wamisionari Wakatoliki Mtandaoni  Tanzania  Kilichoandikwa na Mwandishi na Mahiri  WILLIAM BHOKE

Wamisionari wanawakaribisha  katika semina zitakazo endeshwa na

Padre Titus Amigu – MADA YA SAKRAMENTI YA UPONYAJI

Padre Joseph Mosha  – UMISIONARI NA UTUME WA VIJANA KUPITIA MITANDAO YA KIJAMII

Fr Stephen Kadilo – AFYA NA MALEZI YA VIJANA

Mr Prosper   Magali – MBINU ZA KUKUZA,KUANZISHA BIASHARA (UJASILIAMALI)

Kuanzia tarehe 12 – 13.11.2020

Tarehe 14.11.2020 Itakuwa kilele cha Maadhimisho haya ambayo misa Takatifu na Shughuli mbalimbali

Zitaendelea katika kanisa kuu la Kiaskofu Jimbo kuu la Katoliki la Dodoma  na Baadae Sherehe ya  Kilele  katika ukumbi wa SANTHOME  WA SHULE YA MASISTA WAABUDUO EKARISTI

 

MATANGAZO YA MISA YA UFUNGUZI NA YA KILELE YATARUSHA NA REDIO MARIA TANZANIA LIVE

PI BAADHI YA MITANDAO YA KIJAMII INAYOTUMIKA NA WAMISIONARI HAO MTANDAONI YATARUSHA MADA  NA MATUKIO LIVE.

Imeandaliwa na  Mwenyekiti Wa Kamati ya Mitandao Kitaifa ( Wamisionari Wakatoliki Mtandaoni) Majegero  Selecius,  Edited by Nicolaus